Tuesday, July 31, 2012

LEKA DUTIGITE -KIGOMA ALL STARS ( official video)

BIFU YA RICK ROSS "FREEWAY" NA RICK ROSS RAPPER " BOSS"

Siku kadhaa zilizopita alijitokeza 'Freeway' ambaye inasemekana ndio mmiliki halali wa jina la 'Rick Ross' na kudai kuwa Rapper Rick Ross 'the boss' wa maybach music, amechukua jina lake na kulitumia bila idhini yake. Hivyo jamaa aliamua kuingia mahakamani kumfungulia Rick Ross 'boss' kesi. Na kubwa analodai Freeway anadai kuwa ingekuwa Rapper huyo 'boss' amepitia maisha kama aliyopitia yeye basi isingekuwa ishu kwake,ila imekuwa tofauti kwani 'Boss'haja experience real life aliyopitia yeye. Katika hatua nyingine,leo hii Freeway ameibuka na kusema kuwa anajitahidi kuwazuia washikaji wake wa karibu ambao wanampango wa kumfanyia kitu mbaya Rapper Rick Ross 'boss' wasifanye hivyo. Moja kati ya washikaji waliotaka kuinunua hiyo kesi ni Suge knight ambaye aliwahi kuwa meneja wa hayati 2pac. Freeway 'RickRoss' ameishi maisha ya kitaa sana na kwake yeye jela ilikuwa kama ndo home. Alikuwa real gangsta & hustler.Fuatilia interview yake aliyoifanya hapo chini.

Mwasiti ft Ally Nipishe - Mapito

GELLY WA RYMES-DUUU

KWETU STUDIO YAACHIA SOUNDTRACK YA 'MAISHA SAFARI' YA ERIC MRINDIMA

Hii ni soundtrack ya movie mpya iitwayo 'Maisha safari' inayochezwa na mkali Eric mrindima ambayo ipo jikoni chini ya Muongozaji Mussah Msafiri 'the travellah' wa Kwetu studio. Stay tuned kwa hili.

Saturday, July 21, 2012

HATIMAYE MARIAH CAREY AKUBALI DILI LA KUWA JAJI WA 'AMERICAN IDOL'

Mariah Carey ameonesha kukubali kusaini dili la kuwa jaji wa American Idol. Kwasasa wapo katika hatua za mwisho za kusaini dili hilo. Imewekwa wazi kuwa kama itaenda poa Carey ataweka kibindoni kiasi cha dola milioni 17 za kimarekani ($17 million) kwa msimu mmoja.
Ni siku kadhaa blog hii iliandika kauli ya Nick Cannon ambaye ni Mume Mariah carey akisema kuwa ili kumpata Carey awe jaji ni lazima American idol watoe mzigo wa kutosha, so nadhani wamemsikia. Hongera Carey.

Monday, July 16, 2012

VUNJENI BENKI ILI KUMPATA MARIAH CAREY AMERICAN IDOL,ASEMA NICK CANNON

"Kama American Idol inamuhitaji Mariah Carey kuwa mmoja wa majaji  wao ni lazima wavunje benki" hii ni kauli ya Mr. Carey, Nick Cannon akiongelea point ya Mariah carey,mkewe kuwa mmojawapo wa majaji wa American idol msimu ujao kutokana na waliokuwa majaji Jennifer Lopez na Steven Tyler kutangaza kuwa hawatakuwepo kwenye jopo la majaji msimu ujao. Kauli hii ya Nick inatokana na ukweli kuwa American idol imekuwa haina malipo mazuri kwa majaji wake.
Yap, vipi kibongobongo??????/

BAADA YA 'AMEN' YA MWANA FA, Chukua na hii ' AMEN' - MEEK MILL ft. DRAKE

Hii ni official video ya mkali kutoka Maybach Empire,Meek Mill akimshirikisha Drake kutoka YMCMB. Ngoma inaitwa 'Amen', ni siku kadhaa Mwana FA nae ametoa ngoma ikiitwa 'amen' hivyohivyo, Inakuaje idea zinagongana???? Anyways, yote maisha.

RONALDINHO ATOSWA NA COCACOLA BAADA YA KUKUTWA AKINYWA PEPSI HADHARANI

Mkali wa soka kutoka brazil, Ronaldinho 'Gaucho' amemwagwa na kampuni ya vinywaji baridi ya Cocacola aliyoingia nayo mkataba  wa kuitangaza brand hiyo mara baada ya kupigwa picha akiwa ameshika kopo la kinywaji cha Pepsi likiwa na mrija ambayo ni wapinzani wakubwa wa kibiashara na Coke.
Dinho amekutwa na dhahma hiyo alipokuwa kwenye press conferece na kujikuta aki2pia kitu cha pepsi,na waandishi kama kawaida yao hawakufanya ajizi wakamfotoa mchizi na kumsababishia kumwaga udhamini wa £500,000.
 Ronaldinho hivi karibuni amekuwa kivutio kwa waandishi wa habari kutokana na kuingia kwenye migongano na timu yake aliyokuwa anaichezea ya  Flamengo na kuamua kuingia mkataba na timu nyingine ya  AtlĂ©tico Mineiro miezi miwili iliyopita.

KANYEWEST & KIM KARDASHIAN WAISHI KAMA MAPACHA HIVI SASA

Kanyewest na Mpenzi wake Kim Kardashian hivi sasa wanaishi kama mapacha vile.
Hii ni kutokana na namna ya mienendo yao kufanana kwa siku kadhaa mfululizo. Hivi sasa kim na kanye wakitoka wanavaa nguo zinazo fanana rangi,muda wote wapo pamoja wakishikana mikono. Kila umuonapo Kim basi na Kanye yupo. Hiyo imepelekea kubatizwa jina la 'Kimye',ikimaanisha kim na kanye.
Ofkouz inapendeza, all the best 'Kimye'.

Sunday, July 15, 2012

MICHAEL SCOFIELD,MKALI WA 'PRISON BREAK'

Ofcourse, nani asiyezijua series za Prison break? Ni series ambazo ni kali na nathubutu kusema kuwa hazichoshi hata kuzitazama.

Star wa series hizo ,Michael Scofield hasa ndo ambaye ameweza kuziweka katika umaarufu huo kutokana na umahiri anaouonesha mle ndani. Kwa upande wangu mimi nampa heshima michael popote alipo. Kwa wasanii wachanga kunamengi ya kujifunza kutoka kwake.

MTOTO WA RAMBO AFARIKI AKIWA NA UMRI WA MIAKA 36,

Mtoto wa kiume wa Star wa movie za kibabe,Sylvester Stallone (RAMBO) aitwaye Sage Stallone, amefariki juzi Trh 13/07/2012 akiwa na umri wa miaka 36.

Sababu za kifo chake bado hazijafahamika wazi ingawa ripoti za awali zinaonesha kuwa alikuwa nyumbani kwake na girlfriend wake au mfanyakazi wake wa ndani.Baada ya watu wa afya kuja pale wamesema kuwa kifo kimesababishwa na matumizi ya madawa ya kulevya,ingawa bado haijathibitishwa zaidi juu ya hilo.

Sage alishawahi kucheza filamu na baba yake iitwayo Rocky 5.

Friday, July 6, 2012

BLACK RHYNO NA MKEWE BAADA YA NDOA


KANYE WEST KUACHIA ALBUM MPYA,PRODUCER WAKE AFUNGUKA

Mkali Kanye west,kutoka G.O.O.D Music family anatarajia kuachia album mpya hivi karibuni. Hayo yamebainishwa na Producer wake No I.D alipokuwa akifanya mahojiano na MTV.
Producer huyo amesema kuwa fans wa Kanye wakae tayari kupata album hiyo ikiwa ni kama double dose kwani album yake ya  'summer cruel' bado ipo sokoni.
No I.D amesema wapenzi watarajie vitu bomba.

ONE INCREDIBLE - DEBUT VIDEO by DUKE GERVALIUS

Wednesday, July 4, 2012

SHILOLE KU- SHOOT VIDEO MPYA,KWETU STUDIO YAHUSIKA

Mdada mwenye vipaji kibao vikiwemo vya muziki na uigizaji Shilole,kufanya  video  ya wimbo wake uitwao VIUNO TUCHEZE ambao amewashirikisha richard mavoko na kitokololo.  .
Video hiyo inatarajiwa kufanywa na studio inayokuja juu katika utengenezaji wa video kali,Kwetu studio iliyopo DSM.


ERIC MRINDIMA,MKALI WA COMEDY, KUJA NA 'MAISHA SAFARI'

Mkali wa Comedy Eric Mrindima,ambaye bado anandoto za kufanya mengi mazuri anatarajia kuachia 'short film' yake iitwayo "Maisha safari". Mpango huo unasimamiwa kwa karibu na Kwetu studio ya Jijini Dsm.
Hizi ni baadhi ya picha zilizopigwa wakati wa harakati za upikaji hiyo kitu.
Hope itakuwa poa, ngoja tuisikilizie.

Monday, July 2, 2012

MTANGAZAJI WA CNN, ANDERSON COOPER AJITANGAZA KUWA NI SHOGA

Mtangazaji wa vipindi vya LIVE wa CNN  Anderson Cooper leo ameweka wazi kuwa yeye ni shoga na ataendelea kuwa shoga.
Amebainisha hayo kupitia e-mail ndefu aliyomtumia mwandishi wa Daily Beast, Andrew Sullivan, ambapo amesema kuwa muda wote alikuwa anaandika na kutangaza mambo ya wengine na sasa umefika wakati wa yeye kuandikwa na kutangazwa.

Amesema kuwa alikuwa hayupo comfortable kukaa na siri hiyo moyoni.Sehemu ya email hiyo ilisema : "The fact is, I'm gay, always have been, always will be, and I couldn't be any more happy, comfortable with myself and proud," ...... "I am also blessed far beyond having a great career. ... I love, and I am loved."Alisema Cooper.
 Stori hii imetolewa hapa

CATRINA, THE COMING SUPER STAR IN TZ,AFUNIKA ARUSHA,AWA MC SHUJAA FIESTA 2012

CATRINA MWANAMUZIKI MKALI MWENYE KIPAJI CHA KUIMBA KUTOKA MKOA WA ARUSHA,BAADA YA MUDA MFUPI ATAKUWA MOJA KATI YA WANAMUZIKI BORA.video yake inaitwa KARIBU YANGU imerekodiwa na kwetu studios.na nimshindi wa MC SHUJAA wa FIESTA 2012 arusha.
Stay tuned.

JAY-Z,KANYE WEST,BEYONCE WA 'SHINE' TUNZO ZA BET 2012

Tunzo za BET zimefanyika usiku wa jana jumapili ikiwakutanisha wakali kibao wa burudani,lakini kubwa zaidi ni show kali zilizo pigwa na wakali kadhaa wakiwemo kanye west,Nicki minaj,2chainz,Rick Ross na kundi lake la Maybach Music,melanie fiona na wakali wengine kibao.
Katika usiku huu wa tunzo za BET zimekuwa nzuri zaidi kwa Kanye West,Beyonce na Jay-Z kwani wame shine ile mbaya na imefurahisha zaidi pale iliposemekana Mtoto wa Beyonce na Jay-Z aitwaye BlueIvy  carter kuwa amepata toy mpya za kuchezea,’wakimaanisha zile tunzo ndio toys’.
Show iliongozwa vizuri na actor mkali Samuel L. Jackson.

 Soma list ya washindi hapa chini:

Best Group: The Throne (Kanye West & Jay-Z)
Best Actor: Kevin Hart
Best New Artist: Big Sean
Best Male R&B Artist: Chris Brown
Best Collaboration: Wale ft. Miguel
Best Gospel: Yolanda Adams
Best Female R&B Artist: Beyoncé
Best Female Hip-Hop Artist: Nicki Minaj
Lifetime Achievement Award: Maze featuring Frankie Beverly
Video Of The Year: “Otis,” The Throne (Kanye West & Jay-Z)
BET Humanitarian Award: Rev. Al Sharpton
Viewers’ Choice Award: Mindless Behavior
Video Director Of The Year: BeyoncĂ© & Alan Ferguson
AOL Fandemonium Award: Chris Brown

Fid Q ft Yvonne Mwale - Sihitaji Marafiki(official video)

Sunday, July 1, 2012

JOHN CENA ATIMIZA MIAKA 10 NDANI YA WWE,AONGELEA MAISHA YAKE

Mkali wa mieleka, John Cena atimiza miaka kumi tangu aanze mchezo huo tarehe 27 June 2002. Kwa kipindi chote hiko cha miaka 10 Cena amekuwa gumzo kwa kila rika kutokana na umahiri wake katika mchezo huo. Amekuwa ni kipenzi na kivutio cha wengi.
Akielezea maisha yake ya mieleka, Cena anaikumbuka mechi yake ya kwanza iliyofanyika June 27 2002 dhidi ya Kurt Angle ambapo anasema kuwa alipata kiraruraru ingawa kwake ndo siku pekee historia ilipoanza andikwa.Kuhusu mafanikio Cena amesema kuwa kuendesha maisha kupitia mchezo huo ndo mafanikio yake. Amesema kuwa hakutarajia hata siku moja kuwa angefikia level aliyofikia leo.

CHRIS BROWN AM DISS DRAKE KWENYE FREE STYLE,AKITUMIA BEAT YA 'I DONT LIKE'

click here to listen The Game & Chris Brown - I Dont Like Rem.. 
 Baada ya ugomvi mkubwa kati ya Chris Brown na Drake uliotokea wiki mbili zilizopita kwenye night club na ambao hadi leo bado chanzo halisi cha ugomvi huo haujafahamika, ingawa unahusishwa na kumgombania mdada Rihanna, Leo hii Chris brown akiwa na The Game wameachia freestyle ambayo ime m-diss Drake moja kwa moja. Baadhi ya mistari hiyo ni kama hii hapa
 " fuck niggaa,that's that shit i dont like
,They throwing bottles/I'm throwing models, just cause i give bitch long pipe."
 kama vp download hii freestyle uisikie ambayo imechanwa na chris brown akiwa naThe Game kupitia beat ya 'Chief keef' ya ngoma  iitwayo 'I dont like'.pia waweza ingia hapa usome mashairi yote ya ngoma hii http://www.youtube.com/watch?v=tYjcYIG6q9Q