Thursday, June 28, 2012

Hurt Somebody- Akon Feat. French montana.mp3


 click here to download  Hurt Somebody- Akon Feat.french montana .mp3 

CHRIS BROWN & DRAKE KUPEWA $ MIL.1 KILA MMOJA IWAPO WATAZICHAPA LIVE KWAAJILI YA 'CHARITY'

Wakali Chris Brown na Drake wameahidiwa ofa ya Dola milioni moja kwa kila mmoja iwapo wataafiki wazo la kuzichapa live ulingoni kwaajili ya kuchangia mfuko wa hisani 'charity'.
 Kwa mujibu wa promota wa wazo  la mpambano huo,Damon Feldman, amesema kuwa pambano litakuwa ni la raundi tatu na ameongeza kuwa atatoa kiasi hichohicho cha fedha iwapo Mdada Rihanna ambaye inasemekana ndio chanzo cha bifu la Brown na Drake, atakubali kuwa 'Ring girl' wa pambano hilo.
“It’s more of a show than anything, and we can raise millions for charity, “Instead of fighting in a bar, they could get paid to fight!""We would like to have Rihanna as a ring girl, as well, but if she doesn’t take our offer, we know she will be watching,”
Hii story ni kwa mujibu wa thehollywoodgossip.com


Belle9 - Amerudi ( Official video) DJ Charzjoe

Wednesday, June 27, 2012

PICHA YA Dkt. ULIMBOKA BAADA YA KUOKOTWA


P-Square - Beautiful Onyinye ft. Rick Ross [Official Video]

Snoop Dogg na mwanae Cordell Broadus, Beautiful photo

Baba na Mwana, they look nice,isn't it? ofkouz it's.

MKONGWE WA FILAMU KUTOKA BOLLYWOOD INDIA,AMITABH BACHCHAN AZUSHIWA KIFO

Mkongwe wa tasnia ya filamu kutoka Bollywood India, Amitabh Bachchan Azushiwa kifo na blog moja ambayo inasemekana ndiyo blog pekee iliyowahi kutangaza vifo hewa vya mastaa wengi wakiwemo David Beckham, Justin Bieber n.k
Blogger huyo ametangaza kifo hiko jana akisema kuwa Amitabh amefariki kwa ajali ya gari.
Habari za kifo hiki zimekanushwa Kupitia mtandao wa http://www.deccanchronicle.com na hadi sasa hivi Amitabh bado haja comment kitu chochote kutokana na uzushi huo.

Dkt. STEPHEN ULIMBOKA AOKOTWA PORINI AKIWA TAABANI

Mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari nchini, Dk Stephen Ulimboka amelazwa katika hospital ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuokotwa katika pori la Pande nje kidogo ya jiji akiwa taaban.Inasemekana Dk Ulimboka alitekwa jana na watu wasiojulikana.
Hii stori ni kwa mujibu wa Mwananchi communication na picha ni kwa mujibu wa blog ya leotainment.

Tuesday, June 26, 2012

EXCLUSSIVE: 50 CENT APATA AJALI YA GARI

Curtis Jackson '50 Cent' amepata ajali ya gari iliyotokea jana usiku baada ya Gari yake ambayo ni Bullet proof "SUV" kusukumwa na Lori kubwa mjini New York.
Kwa mujibu wa mtandao wa This is 50, 50 kwasasa ameshatoka hospitali ambapo alikimbizwa mara baada ya ajali na alipatiwa vipimo vya shingo na mgongo.

Katika ajali hiyo pia Dereva wake amejeruhiwa..



Izzo Bizness ft Shapsin - Mwaka Jana ( Official Video )

Wednesday, June 20, 2012

BAADA YA UKIMYA MREFU,MIKE TYSON AFUNGUKA,ASEMA "NILIKUWA MTU WA 'MALAYA' "PROSTITUTE HUNTER"

The heavy weight Mike Tyson,baada ya ukimya mrefu leo amefunguka katika kipindi cha live kupitia runinga ya NBC na kusema kuwa maisha yake ya zamani yalikuwa ni ya kutafuta malaya na kulala nao "prostitute hunter".
Kupitia kipindi hiko cha runinga, Tyson ametiririka mambo yake mengi ya kipindi cha nyuma, na kufanya audience kuwa surprised.
Kuanzia mwezi ujao, July 31 Mchizi atakuwa na show yake mpya kwenye runinga itakayoitwa "Mike Tyson: Undisputed Truth." ambayo itaweka wazi mambo kibao ambayo wengi hawakuyafahamu kabla.

Saturday, June 16, 2012

SANDU GEORGE, "KID BWOY" AONGEZA IDADI YA MAPRODYUZA BONGO DSM

Sandu George, maarufu kama Kid Bwoy, ameongeza idadi ya watayarishaji muziki ndani ya jiji la Dar es salaam baada ya kuhamisha studio yake akitokea Mwanza kuja Dar.

Mhunzi wa sauti huyo ambaye pia alikuwa mtangazaji wa kituo cha RFA , kwasasa unaweza kumsikiliza kupitia Tone radio mtandaoni.
Kazi kwenu wasanii.


Exclusive: Hermy B aeleza kilichotokea kati yake n...

 Exclusive: Hermy B aeleza kilichotokea kati yake n...: Hermy B kulia akiwa na MC wa TPF Tarehe 23/05/2012 tuliandika makala inayosema: ‘Ay na B’Hits na urafiki uliochuja kimya kimya...

EXCLUSSIVE: BIRDMAN AFUNGUKA JUU UGOMVI WA DRAKE NA CHRIS BROWN,ASEMA DRAKE HAKUFANYA KITU CHOCHOTE KIBAYA

Bosi wa YMCMB, Bryan Williams "Birdman" ametoa kauli yake kufuatia fujo na ugomvi kati ya Drake na Chris Brown uliotokea juzi kati. Birdman kasema kuwa Drake sio mtu wa fujo za aina hiyo hivyo anaamini hajafanya kitu chochote kibaya kwenye fujo hizo.
Kwa maneno yake alisema hivi pindi alipokuwa akihojiwa na MTV ""Well, to me, I think n---as got Drake twisted. A lot of n---as be playin', pitty-pattin' with Drake. I don't like that sh--, period,. "Drake is one of us, so if you f---in' with Drake, you f---in' with us, period!"
"To me, Drizzy ain't did nothin' wrong, he ain't done nothin' wrong to nobody. He just doin' great music," . "He's not a reckless guy out there just wildin' out; he's a humble kid makin' great music." Alisema Birdman akimtetea msanii wake wa YMCMB.
Fujo zilitokea juzi trh 15/6/2012 kwenye night club ya W.I.P huko NYC zikimhusisha Drake na wenzake kuwashambulia kina Chris Brown kwa Chupa za moto na kusababisha majeruhi kadhaa wakiwemo mcheza mpira wa kikapu NBA Tony Parker pamoja na mlinzi wa Chris Brown.
Polisi inaendelea na uchunguzi na inasemekana Drake bado yupo huru hadi upelelezi ukamilike.

HALI YA MZEE SMALL YAWA TETE,TUMUOMBEE

Hali ya Msanii mkongwe wa filamu na vichekesho nchini Tanzania,Mzee Small imekuwa mbaya kiasi cha kuhamishwa hospitali ya Amana alipokuwa mwanzo na kupelekwa Muhimbili kwa matibabu zaidi,na kwa mujibu wa Global publisher Mzee small ameruhusiwa kurudi nyumbani lakini bado hali si nzuri. Tumuombee awefresh

YOUNG D AMWAGA CHOZI LIVE REDIONI BAADA YA KUKUMBUSHWA MWANZO WAKE WA MUZIKI

Young D, Young Dar es salaam,Young rapper, Dee Leo mchana amemwaga chozi Live redioni katika kipindi cha Bongo fleva cha clouds FM baada ya presenter Adam Mchomvu, Baba Jonii,kum surprise kwa kumsikilizisha clip ya interview yake ya kwanza kabisa alipoanza muziki.
Akiongea akiwa katika hali ya kwikwi ya kilio, Dee amesema kuwa mara ya mwisho kulia ilikuwa baada ya kifo cha baba yake na hii ya leo imemkumbusha vitu vingi sana vya nyuma kiasi ya kwamba ameshindwa kujizuia na kumfanya asiendelee na interview hiyo na kumuacha Mchomvu akiongea na mtu aliye ambatana na Dee ambaye anamfahamu vizuri.

BAADA YA KUMWAGWA TIP - TOP, DOGO JANJA AFUNGUKA. ASEMA MUNGU NDO ATAKAYEMLIPA

Wiki hii imekuwa hot kwa Dogo Janja Baada ya mtu pekee aliyemleta Dar na kumuunganisha na Kundi la Tip-Top, Madee, kumtosa rasmi na kumrudisha kwao Ngarenaro, A.city.
Yameongelewa mengi na Madee pamoja na Babu Tale ambaye ndio msimamizi wa Kundi kuhusu Dogo,lakini Leo Dogo kafunguka kuwa Madee sio 'Binadamu' kutokana na dhuluma ambazo amekuwa akimfanyia kwa kipindi chote alichoweza kuwa katika kundi. Amesema kuwa hajawahi kugusa hata senti moja ya albam yake na show zote alizopiga alikuwa anapewa hela ndogo sana,mfano show ya milioni 1 alikuwa akipewa laki mbili tu. 
Kwasasa Dogo yupo homa Arusha na kwa mujibu wa Mma yake mzazi ni kuwa Dogo kapokelewa na wasanii wakali wa Arusha akiwemo JCB kitu ambacho hakukitegemea. Kwa upande wa Baba mzazi wa Dogo amesema kuwa wanaangalia namna ya kuweza kutafuta haki za Dogo.
Kuhusu shule Dogo amesema hakuacha shule ila anafanya taratibu za kuhamia Arusha. Ila kubwa kabisa amesema anaamini Mungu ndiye mlipaji wa mambo yote aliyofanyiwa na Madee/Tip-Top kwani anaamini haki ya mtu haipotei.
Haya yote yamefikia hapo baada ya Madee pamoja na Babu Tale kumshutumu Dogo kuwa amekuwa mtoro wa shule na msumbufu,kitu ambacho kimekanushwa na mama mzazi wa Dogo baada ya kuwasiliana na walimu wa Dogo.





Wednesday, June 13, 2012

FLOYD MAYWEATHER ATUPWA RUPANGO KWA KUMPIGA MAMA WATOTO WAKE MBELE YA WATOTO

Mkali wa ngumi za uzito wa juu duniani, Floyd Mayweathe Jr. ametupwa rupango kwa kosa la kumpiga mama watoto wake mbele ya watoto zao.

Mchizi amepigwa mvua za miezi mitatu kukaa ndani ya mjengo,ingawa jamaa ameiomba mahakama iweze kumruhusu akatumikie kifungo chake kwa siku zilizo salia akiwa nje kwani amekuwa hapati treatment nzuri mle ndani na ana wasi wasi na kushuka kwa uwezo wake wa kutupa masumbwi, kitu ambacho hata daktari wake amesapot.
Ijumaa ijayo mahakama itatoa jibu juu ya ombi la mchizi la kutaka apate kifungo cha nje.

Ameen - MwanaFA feat Dully Sykes and AY.mp3 (DJ Charzjoe)

 Gonga hapa umsikie binamu

 MwanaFA feat Dully Sykes and AY.mp3 

Prezzo & Ally B - Mimi na Wewe

Monday, June 4, 2012

LIL WAYNE AVUNJA SHOW YA NICKI MINAJ KWENYE TAMASHA LA SUMMER JAM LA HOT 97

Bosi wa YMCMB Lil wayne ametangaza kuvunja show iliyokuwa ifanywe na mdada nicki minaj katika tamasha la summer jam lililo andaliwa na kituo maarufu cha hiphop nchini marekani cha Hot 97 baada ya mtangazaji wa kituo hiko Peter Rosenberg ku diss live ngoma ya mdada Minaj iitwayo 'starships'.
Mtangazaji huyo alinukuliwa hivi akiwa live "I know there's some chicks here waiting to sing 'Starships' later, I'm not talking to y'all right now. F--- that bullsh--. I'm here to talk about real hip-hop sh--,"
Kutokana na hilo Weezy hakuvutiwa na hizo comment za mtangazji huyo hivyo akaamua ku twit kupitia akaunti yake  "Young Money ain't doing summer jam,"

Kabla ya hapo Nicki alishatangaza kupitia mtandao wa twitter kuwa angeenda na kupafomu na wakali kibao kwenye show hiyo wakiwemo Cam'ron, 2 Chainz, Nas, Lauryn Hill, reggae star Beenie Man, Foxy Brown, Lil Wayne na members wengine kibao wa Young Money/Cash Money family.

Hii sio mara ya kwanza kwa mdada Nicki kupata Diss juu ya uwezo wake katika hiphop, mwezi wa april baada ya  kuachia albamu yake ya sophomore Minaj alizungumza na MTV na alifunguka juu ya maisha yake ya kitaa kabla ya umaarufu na alimalizia kwa kusema "I'm still me, hip-hop culture is still in my heart, That can never leave me."




BAADA YA KUZUSHIWA KIFO D'BANJI AFUNGUKA

Baada ya kuzushiwa kifo mkali kutoka Nigeria Dapo Oyebanjo a.k.a D'Banj amefunguka kupitia akaunti yake ya twitter na kukanusha uzushi huo na kusema kuwa yuko mzima na afya tele.Aliandika haya maneno Pls ignore the nonsense rumours. I’m very much alive and well! Thanks be to God! Thank you 4 all ur concern‘ .
Habari zilizozushwa zilisema kuwa mchizi alipigwa risasi na watu watatu wasiojulikana alipokuwa anatoka Atlanta kwa bosi wake wa G.O.O.D Music Kanye west na kukimbizwa hospitali ya st.Joseph ambako alifariki baada ya dakika chache kutokana na maumivu.