Wednesday, November 20, 2013

A.Y AAMUA KUTIMIZA NDOTO YA KUWA RUBANI,AINGIA SHULE RASMI.

Ni ngumu sana kwa mtu maarufu, mwenye hela na uwezo wa kilakitu anchohitaji kuamua kutimiza ndoto
aliyokuwa nayo kitambo. Lakini hii inaenda kutokea kwa mkali A.Y 'Ambwene Yesaya' ambaye ameamua kurudi Chuo na kufanya kitu ambacho alikuwa anakitamani long time kitambo. Lakini hii haimaanishi kuwa mchizi anaacha muziki. Kwasasa A.Y amesha lipa ada ya hiyo kozi katika  Chuo cha Mafunzo ya Urubani cha ‘Mosswood Aviation Academy’ kilichopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA) na anatarajia kuanza masomo Januari 2014.Amefunguka hayo kupitia Mwananchi Hili ni bonge la concept kutoka kwa mchizi na ni mfano bora. All the best bro.

Thursday, October 31, 2013

Mariah Carey na Nas wapiga collabo kali

Mapema Mwaka huu Mdada Mariah Carey aliweka teaser juu ya albam yake ijayo iitwayo 'The Art of Letting Go', lakini alichelewa kuiachia hiyo albam kama alivyoahidi ili kukamilisha mambo kadha wa kadha. Moja kati ya hizo sababu za ukamilishaji ni pamoja na kuijumuisha ngoma anayofanya na Mkali Nas.Naamini itakuwa ni bonge la collabo.Msikilize yeye mwenyewe Mariah Carey akifunguka.

Tuesday, October 29, 2013

EMINEM NA RIHANA KUFANYA NGOMA MPYA YA PAMOJA TENA 'MONSTER''

Kwa mara ya kwanza Rihana 'Riri' na Eminem walitisha sana kwa ngoma ya 'Love the way you lie', Jana October 28, Eminem ameweka wazi kuwa wanaachia ngoma nyingine iitwayo 'Monster' ambayo inatabiriwa makubwa katika soko.
Ngoma inaanza kwa Acoustic guitar na Rihana ananzaa kwa kuimba maneno haya "I'm friends with the monster that's under my bed/ Get along with the voices inside of my head/ You trying to save me, stop holding your breath," Ni ngoma kali in short.

CHRIS BROWN AACHIWA BAADA YA KUSOTA JELA MASAA 36

Hatimae Chris Brown ameachiwa huru baada ya kusota jela kwa zaidi ya masaa 36 kutokana na shambulio alilolifanya kwa mtu nje ya Night Club.
Breezy na Bodyguard wake walikamatwa Juzi Jumapili asubuhi baada ya kumchapa jamaa aliyefahamika mahakamani kwa jina la Parker Adams mwenye umri wa miaka 20. Jamaa amesema mahakamani kuwa alikuwa anataka kupiga picha na Breezy ghafla akastukia akitupiwa sumbwi na breezy.
Kwa mujibu wa Mahakama Chris Brown na Bodyguard wake wamekutwa hawana hatia na wameachiwa huru.ila wameamriwa kurudi mahakamani Novemba 25 na kukaa umbali wa yard 100 na jamaa aliyewashtaki.

Monday, October 28, 2013

Kwanini Jay-Z na NAS ni mfano wa kuigwa kwenye Hip hop???

Wakali ambao wana historia za kipekee kwenye ulimwengu wa Hip hop Nasir Jones Escoba 'Nas' na Sean Carter 'Jay -Z' ni mfano mzuri wa kuigwa katika ulimwengu wa Hip hop. 
2005- Ulikuwa ni mwaka ambao kulikuwa na bifu kali ya Jay-Z na Nas katika ulimwengu wa Hip hop. Baada ya Jay-Z kumponda Nas kwenye tamasha la Summer Jam 2001 na kutoa album aliyoiita 'Take over' to the world, Jay Z na Nas waliingia kwenye vita kali ya mashairi,kama vile Take over ya Jay-Z vs Ether ya Nas, Ether vs Super Ugly, Super ugly vs The Last Real Nigga Alive na Blue print2.  Kilichofurahisha katika bifu ya Jay Z na Nas ni kwamba bifu ilitengeneza Great Music na haikuwa kama bifu zinazo ibuka miaka ya hivi karibuni. Na bifu ya Jay na Nas ndo bifu ambayo kwa upande wangu nadhani inafaa kuwa mfano kwa wasanii wasasa wa Hip hop.
Mnamo October 27, 2005, katika tamasha la Powerhouse Concert  lililoandaliwa na  kituo cha radio 105.1 ndipo ambapo bifu ya Jay-Z na Nas ilikua officialy squashed pale Nas alipo tokea kwenye show ya Jay-Z bila kutarajiwa. Na hapo kwa makusudi jina la show likabadilika na kuitwa 'I declare War' yani 'Natangaza Vita'. Watu wengi mashabiki wa Jay walitegemea Jay angejipanga kwa mashairi ya vita dhidi ya adui yake 'Nas'. Badala yake Jay-Z aligeuka na kupanda stejini akiwa na adui yake Nas na kuperform ngoma ya 'Dead Presidents' na 'The World is Yours'. Baada ya Performance Jay na Nas wakapeana mikono na ukawa ndo mwisho wa Bifu yao. Hapo ndipo unapata picha kuwa ile 'I Declare War' ni kinyume cha 'I Declare Peace'.
Mnamo Januari 2006,  Jay-Z na Nas  wame make headlines baada ya Jay kumsaini Nas kuingia Def Jam wakati Record label ikiwa chini ya Hov. 'Jay-Z'.  Nas aliendelea kushirikiana na Jay  katika  album ya Hip hop is dead  kupitia ngoma ya 'Black Republicans' na kwa mara nyingine mwaka 2007 wametoa ngoma ya 'Success'.
Huu ni mfano mzuri kwa wana hip hop wa sasa kujifunza namna ya bifu za kujenga.

CHRIS BROWN ATIWA NGUVUNI KWA KUMTUPIA MASUMBWI MTU

Mkali Chris Brown 'Breezy' Jana mida ya saa 4 asubuhi amekamatwa na makachero kwa kosa la kumchapa makonde jamaa mmoja ambaye inasemekana hawajuani. Taarifa zilizopatikana kutoka mtandao wa TMZ zinasema Mchizi Breezy aliingia kwenye majibizano na mchizi mwingine nje ya Hotel, huku na huku Breezy si  akamrushia jamaa Konde la uso na inasemekana aliyepigwa hajarudishia mashambulizi. Breezy alikamatwa na kutupwa sero akiwa na Bodyguard wake.
Breezy bado yupo kwenye maangalizi ya kesi ya kumshambulia Rihana na ameongeza ishu nyingine. By the way kinachonishangaza kwa Breezy ni kwamba hivi alimuajira Bodyguard afnye kazi gani iwapo mpango wa ngumi anausimamia mwenyewe. LOL!!!

Saturday, September 14, 2013

Francis Cheka kujengewa nyumba ya Kisasa na Serikali

Baada ya kumtwanga Mmarekani Phil Williams katika Masumbwi na kutwaa ubingwa wa Dunia, Mkali Francis Cheka sasa kujengewa nyumba ya kisasa na serikali kama sehemu ya pongezi kwa ushindi huo.
Ahadi hiyo imetolewa Jana Trh. 13 Sept. 2013 na Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mh. Joel Bendera kwa niaba ya serikali wakati wa hafla fupi ya kumpongeza Mkali huyo Mjini Morogoro. Hongera sana Cheka. U deserve Bro.

Saturday, August 24, 2013

Kendrick Lamar kajitokeza katika categories 14 katika BET Hip Hop Awards 2013

BET Imetangaza nomination za tuzo za hip hop 2013 na kumuweka Mkali Kendrick Lamar katika Categorie 14 akifuatiwa na Drake categories 13 na J-cole 10. BET mwaka huu inatarajiwa kuwa hosted na Snoop Lion, na show inatarajiwa kurekodiwa September 28 na kurushwa hewani October 15 mwaka huu.

Check out the full list of nominees:
Best Hip Hop Video: A$AP Rocky f/ Drake, 2 Chainz & Kendrick Lamar – Problems,  B.o.B f/ T.I. & Juicy J – We Still In This,  J. Cole f/ Miguel – Power Trip, Drake – Started From The Bottom, Kendrick Lamar – Don’t Kill My Vibe
Reese’s Perfect Combo Award (Best Collabo, Duo or Group):  Ace Hood f/ Rick Ross & Future – Bugatti, A$AP Rocky f/ Drake, 2 Chainz & Kendrick Lamar – Problems, J. Cole f/ Miguel – Power Trip, French Montana f/ Rick Ross, Drake & Lil Wayne – Pop That, Kendrick Lamar f/ Drake – Poetic Justice, Wale f/ Tiara Thomas – Bad
Best Live Performer: 2 Chainz,  J. Cole, JAY Z, Kendrick Lamar, Kanye West
Lyricist of the Year: J. Cole, Drake, JAY Z, Kendrick Lamar, Wale
Video Director of the Year: A$AP Rocky & A$AP Ferg, Benny Boom, Director X, Dre Films, Hype Williams
DJ of the Year: DJ Drama, DJ Envy, DJ Funkmaster Flex, DJ Khaled, DJ Scream
Producer of the Year: J. Cole, Hit-Boy, DJ Mustard, Mike WiLL Made It, Pharrell Williams
MVP of the Year: 2 Chainz, J. Cole, Drake, JAY Z, Kendrick Lamar
Track of the Year: Power Trip – Produced by J. Cole (J. Cole f/ Miguel),  Problems – Produced by Noah “40” Shebib (A$AP Rocky f/ Drake, 2 Chainz & Kendrick Lamar), Don’t Kill My Vibe – Produced by Sounwave (Kendrick Lamar), Bugatti – Produced by Mike WiLL Made It (Ace Hood f/ Rick Ross & Future), Started From The Bottom – Produced by Mike Zombie & Noah “40” Shebib (Drake)
Album of the Year: J. Cole – Born Sinner, JAY Z – Magna Carta Holy Grail, Kendrick Lamar – good kid, m.A.A.d city, Nas – Life Is Good, Wale – The Gifted
Who New? Rookie of the Year: Action Bronson, A$AP Ferg, Earl Sweatshirt, Joey Bada$$, Trinidad Jame$
Hustler of the Year: Diddy, JAY Z, Kendrick Lamar, T.I., Kanye West
Made-You-Look Award: 2 Chainz, A$AP Rocky, JAY Z, Kendrick Lamar, Nicki Minaj, Kanye West
Best Hip Hop Online Site: Allhiphop.com, Complex.com, GlobalGrind.com, RapRadar.com, WorldStarHipHop.com
Best Club Banger: Ace Hood f/ Rick Ross & Future – Bugatti (Produced by Mike WiLL Made It), A$AP Rocky f/ Drake, 2 Chainz & Kendrick Lamar – Problems (Produced by Noah “40” Shebib), Drake – Started From The Bottom (Produced by Mike Zombie & Noah “40” Shebib), French Montana f/ Rick Ross, Drake & Lil Wayne – Pop That (Produced by Lee on the Beats), Trinidad Jame$ – All Gold Everything (Produced by M.e. (Devon Gallaspy)
Best Mixtape: Big Sean – Detroit, Chance The Rapper – Acid Rap, Travi$ Scott – Owl Pharaoh, Stalley – Honest Cowboy, Trinidad Jame$ – Don’t Be S.A.F.E.
Sweet 16 (Best Featured Verse): Diddy – Same Damn Time (Remix) (Future f/ Diddy & Ludacris), Drake – Versace (Remix) (Migos f/ Drake), Future – Bugatti (Ace Hood f/ Rick Ross & Future), Kendrick Lamar – Problems (A$AP Rocky f/ Drake, 2 Chainz & Kendrick Lamar). Wiz Khalifa – U.O.E.N.O. (Remix) (Rocko f/ Future & Wiz Khalifa)
Impact Track: J. Cole f/ TLC – Crooked Smile, JAY Z f/ Justin Timberlake – Holy Grail, Macklemore & Ryan Lewis – Same Love, Wale f/ Sam Dew – LoveHate Thing, Kanye West – BLKKK SKKKNHEAD
People’s Champ Award: A$AP Rocky f/ Drake, 2 Chainz & Kendrick Lamar – Problems, J. Cole f/ Miguel – Power Trip, Drake – Started From The Bottom, Kendrick Lamar – Don’t Kill My Vibe, Macklemore & Ryan Lewis f/ Mary Lambert – Can’t Hold U.

Kanye West aweka hewani picha ya kwanza ya mtoto wao Tangu azaliwe


Baada ya miezi miwili ya matazamio yetu, hatimaye picha ya kwanza tangu kuzaliwa kwa mtoto North West, imewekwa hewani na baba wa mtoto ambaye ni Kanye West himself. Mtoto North West alizaliwa June 15 mwaka huu, na kwa kipindi hiko chote wazazi hao "Kanye West na Kim Kardashian" hawajawahi kuweka hewani picha ya mtoto wao hadi jana Ijumaa kupitia kipindi cha television cha Kris Jenner's chat show ambapo Kanye West alikuwa na exclusive interview.


"The Expendables 3" ipo njiani yaja. Cheki picha za uandaaji wake hapa

Mkali Sylvester Stallone 'Rambo' ameanza uandaaji wa filamu ya "The Expendables 3" ambapo safari hii amewaongeza wakali wengine akiwemo mkali Wesley Snipes. Hizi ni baadhi ya picha wakiwa katika uandaaji wa filamu hiyo.






Friday, August 9, 2013

50CENT HAYUMO KWENYE LIST YA UBABA KWENYE CHETI CHA KUZALIWA CHA MWANAE WA DAMU

Mkanganyiko ulitokea kwa 50Cent pindi alipotiwa nguvuni kwa kosa la kushambulia baada ya kumchapa demu wake wa zamani Daphne Joy mwezi uliopita. 50 alikana mashtaka na aliachiwa, lakini kitu cha kushangaza ni kwamba inawezekana mchizi akawa na mtoto na Bi.dada Daphne Joy ambaye hakuwahi kuweka wazi. Mwanasheria kutoka jiji la L.A amefunguka kuwa 50 na Daphne Joy wana mtoto kwa mujibu wa maelezo ya tukio la shambulio lakini wawili hao hawajawahi kuliweka wazi hilo kwenye public, mtoto pekee wa 50 ambaye anajulikana ana umri wa miaka 16 hivi sasa aliyezaa na Mdada Shaniqua Tompkins.
Mtandao wa TMZ Umefanikiwa kunasa cheti cha kuzaliwa cha Mtoto huyo mpya na kukuta sehemu ya jina la baba imeachwa wazi kitu ambacho kinaweza kutafsiriwa kuwa labda Bi. dada Daphne Joy bado hana uhakika juu ya baba halisi wa mtoto au hakupenda tu kumuweka Fif kwa sababu zake zingine. Lakini mtoto huyo bado anatumia jina lake la mwisho kama Jackson 'Curtis' kitu ambacho tunaamini kuwa Mchizi ni baba halisi wa mtoto. Hadi naiandika story hii 50 bado hajatoa comment yoyote juu ya hili.

BEYONCE AAMUA KUNYOA NYWELE, AWA NA MUONEKANO MPYA

Bi. dada mkali kutoka state, Beyonce Knowles ameamua kufuata nyayo za Bi. shosti Rihanna kwa kuamua
kuyatoa yale manywele yake marefu na kubaki na nywele fupi. Kimtindo amebadili muonekano. Alitupia picha katika mtandao wa Instagram wa muonekano wake mpya.

Thursday, August 8, 2013

USHER RAYMOND AFUNGUKA JUU YA AJALI YA MTOTO WAKE

Mkali Usher Raymond amevunja ukimya baada ya kuamua kufunguka juu ya tukio la Mwanae wa miaka 5 la kupata ajali ya kunasa ndani ya swimming pool. Mkali huyo amefunguka kwa kuwashukuru washikaji wawili ambao walifanikisha kumnasua mtoto Usher V kutoka katika pool hiyo.Katika hilo alinukuliwa akisema "I would especially like to thank the two men who saved my son's life, Eugene Stachurski and Ben Crews. They are true heroes and I am deeply grateful to them," Pia amechukua time hiyo kuweza kusema kuwa mtoto kwa sasa yuko poa. Wakati huohuo Demu  wa zamani wa mkali huyo, Tameka Raymond,amemmaindi mchizi juu ya malezi ya watoto wao wawili, bi.dada huyo ameamua kufungua mashtaka akimmaind mwana kwa kutokuwa na muda wa kutosha wa kukaa na watoto kwani muda mwingi hayupo maskani kitu ambacho kina waweka watoto katika hali mbaya kimaadili, dini, afya, elimu na mambo kama hayo.

Tuesday, August 6, 2013

CHRIS BROWN ATANGAZA KUSTAAFU MUZIKI BAADA YA 'X' ALBUM

Mkali Chris Brown ameonesha kukerwa na kesi na mastori yanayoendelea kitaa na ya kuwa yeye ni 'hit  & run' kutokana na umaarufu wake juu ya mademu, na kwa kupitia mtandao wa Twitter mkali huyo ameamua kufunguka kuwa album yake hii itakuwa ya mwisho kwake kwani amechoka. Ameandika post hizi hapa 'Don't worry mainstream America.After this X album, it'll probably be my last album, Being famous is amazing when it's for ur music and talent. I'm tired of being famous for a mistake I made when i was 18. I'm cool & over it!.' Kwa upande wangu bado siamini kuwa mchizi yuko serious, kwani yeye sio wa kwanza kutangaza kuacha muziki na kurudi tena.

Thursday, August 1, 2013

BUSTA RHYMES AONGELEA WAZO LA DJ KHALED KUTANGAZA NIA KWA NICKI MINAJ

Baada ya Dj Khaled kuweka wazi nia yake ya kumtaka Bi. shosti Nicki Minaj, Mkali Busta Rhymes amesema kuwa bado hajapata uhakika kwa kile anachokisema Mchizi (DJ Khaled)kama kimetoka moyoni au la. Ila kwa namna amjuavyo Khaled huwa ni mtu wa masihara ingawa katika kipande cha video alichotangaza nia haoneshi dalili ya masihara. Busta amesema kuwa amekirudia kipande hiko cha video mara 30 na bado anaona kama mchizi yuko serious hivi.

DJ KHALED ATANGAZA NIA YA KUMUOA NICKI MINAJ,

DJ Khaled ameamua kuweka wazi hisia zake za kimapenzi kwa Bi dada Nicki Minaj kupitia MTV .Mkali huyo amefunguka kuwa anampenda Nicki kwa dhati na analengo la kumuoa kabisa. Khaled alisikika akitamka maneno haya "Nicki Minaj, I'm at MTV, I'm going to be honest with you; I love you,I like you, I want you, I want you to be mine..." Kikubwa ninachoweza kujiuliza ni je, Mchizi yupo realy kwa minaj au propaganda???

Friday, May 3, 2013

Petty ft. Godzilla & Steve RnB - Naumia Moyo

Nikki Wa Pilli ft. G Nako - Kubum Kubam

Darasa Ft Winnie - Nishike Mkono ( Official Video )

UTAMU - Dully Sykes ft Diamond & Dimpoz

Karibu Dar - Kala Jeremiah ft Ben Pol

R.I.P Chris "Mac Daddy" Kelly wa KRISS KROSS

Chris Smith, kushoto, na Chris Kelly wa kundi la Kris Kross  1992. Kelly amefariki May 1 akiwa na umri wa miaka 34. Chanzo cha kifo bado hakija julikana lakini inahisiwa kuwa ni matumizi ya madawa ya kulevya.

Pombe yangu- Madee (official video)

Rich Mavoko - One Time (Official Video)

Young Killer Feat. Belle 9 - Dear Gambe (New video 2013)

mama yeyoo - G.Nako Feat Ben Pol (Official Music Video 2013 )

Lady Jay Dee ft. Prof. Jay-Joto hasira ( official video)

G-LUCK-HAYAONEKANI (Official video)

WOSIA WA LADY JAY DEE IKITOKEA AMETUTOKA

Wednesday, May 1, 2013

WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA


Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.

Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.

Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.

Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.
Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao.

Mimi ni msanii tofauti na hao mnaofikiria.
Nadhani mnafahamu tangu niachane na Tuzo zenu mnazo influence nani apate nani asipate, na tangu niachane na Fiesta nilipolipwa laki 8 mara ya mwisho na kuamua kuunda Band ili nijiajiri na kupata shows zangu mwenyewe, ikafanikiwa sana jambo ambalo limewauma na kuamua kufanya kitu cha kuiangusha Band yangu.

Nita survive kwa njia zozote MUNGU alizonipangia.
Wakati bado wote tunapumua na kwakuwa watu hao hawanipendi kabisa, Naamini fika hawataweza kunipenda hata siku nitakapokuwa nimekufa.

Na huu ndio wosia wangu kwa watu hao.
Natambua wanaweza kutumia redio yao kutangaza sana kifo changu na kusema marehemu alikuwa mtu mzuri na pengine kupiga nyimbo zangu kuanzia asubuhi mpaka jioni.

Ila naomba nitamke hivi, siku nikifa CLOUDS FM isipige nyimbo zangu, wala isiongelee lolote kuhusiana na kifo changu.

Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wasihudhurie msiba wangu, na mkiwaona muwapige wame
Enyi mtakaokuwa hai baada yangu.

Kama wamenifitini, na hawajanipenda nikiwa hai
Hakuna haja ya kujifanya kunipenda nikiwa marehemu.
Sina haja wanipende pia kwakuwa mimi sio ndugu yao, Ila ubaya wanaoundeleza mioyoni mwao wanaujua na nina hakika nafsi zao zinawasuta pia.

Niliamua kujiepusha nao miaka mingi na kufanya biashara zangu, nimekaa kimya watu wanafikiri nabebwa lakini sijabebwa chochote sikutaka ugomvi haya mambo yalianza baada ya Album yangu ya pili ya Binti mwaka 2003 nilipojitoa Smooth Vibes chini ya Ruge.
Nilivumilia fitna nikiamini ipo siku yatakwisha lakini naona moto ndio unazidi kuwaka.

Na hii ni kwasababu wanaogopa msanii akiwa mkubwa watashindwa kumuamrisha, Hamuwezi kumiliki dunia..
Kama mnasema mlinibeba mbona hamkuwabeba dada zenu wa tumbo moja waimbe ili hela irudi nyumbani??. kama kweli wewe Kusaga unajua kubeba basi beba jiwe liimbe liwe star..

Kwa roho zenu mbaya mnaweza kumbeba mpita njia nyie??.
Talent haibebwi, hujibeba kama mnabisha si mna watoto wabebeni basi wawe kama kina Diamond ndio nitaamini kweli nyie mnaweza kubeba watu.

Mnawatishia wasanii kuwa yoyote atakaefanya nyimbo na mimi hazitapigwa, vikao vinne mmeshakaa kunijadili.
Mnadhani je! nitapungukiwa nini endapo wasanii wengine wakiacha kufanya kazi na mimi?? nyimbo hazitakuwa nzuri.
Basi sawa ngoja tuone MUNGU ni nani, Binadamu nani??
Kwahiyo mtaamrisha watu pia wasikae na mimi??

Ilikuwa niseme majina matatu huyo mmoja nimemsamehe baada ya kugundua sio hiyari yake ila yuko under influence ya hawa jamaa wawili.

Kila siku mnamsingizia Ruge peke yake Kusaga ni mfitini kuliko hata huyo Ruge, watu hamjui tu.
Mtu hela zote hizo bado shillingi mbili ya Jide inakuuma??
Roho gani hiyo??

Naishia hapo na sitabatilisha kauli yangu

JIDE

Tuesday, March 5, 2013

LIL' KIM KURUDI UPYA KWENYE GEMU, AMTAMBULISHA TIFFANY FOX KUNDINI

Mwanadada Lil' Kim 'Queen Bee'usiku wa kesho jumatano kupitia 'rapfix live' mtv, anatarajiwa kumtambulisha Tiffany Fox katika timu yake mpya ambayo inatarajiwa kupiga kazi pamoja. Katika show hiyo Kim atakuwa na mkali mwingine mkongwe Talib Kweli. Hii ni katika kuwahakikishia fans wake kuwa anakuja upya. Fuatilia show hiyo usiku wa kesho Mtv.

Rihanna - Stay ft. Mikky Ekko

Tuesday, February 12, 2013

Solo Thang ft. Chid Benz- Viini Macho mp3.

Huu ni ujio mpya wa mkali wa hip hop ambaye muda mwingi amekuwa mtoni katika harakati zake huku akitupia track za hapa na pale. Anajulikana kama Msafiri Kondo maarufu kama Solo Thang 'the Travellah' ambaye kwasasa ametoka na ngoma hii hapa ambayo kamshirikisha mkali mwingine kutoka Ilala Chid Benz. Ngoma inaitwa Viini Macho. Kama hujaipata bado Bonyeza HAPA

Rapper Common asema Apatikane Papa Mweusi Baada ya kutangaza kujiuzulu kwa Papa Benedict XVI

Rapper Common, ameonesha wazi hisia zake za kuhitaji kupatikane Kiongozi mpya wa wakatoliki duniani ( Papa ) mwenye asili ya kiafrika mara baada ya papa Benedict XVI kutangaza kujiuzulu wadhifa huo ifikapo tarehe 28 februari 2013. Rapper huyo ameongea hayo alipokuwa ameulizwa na TMZ juu ya kujiuzulu kwa papa Benedict xvi na mtazamo wake juu ya hilo. Na alipoulizwa nani anaweza kukaa kwenye nafasi hiyo Common hakusita kumtaja Kadinali Peter Turkson kutoka Ghana kuwa anaweza kushika nafasi hiyo. "electing a black Pope would be a beautiful thing" alisema Common.

Whaddup- LL Cool J ft. Chuck D, Travis Barker, Tom Morello & DJ Z-Trip

Ni ujio mpya wa legend wa hip hop, LL Cool J. Hii ni ngoma ambayo inapatikana katika albam yake mpya iitwayo 'Authentic'.
Jamaa anaonesha uwezo wake ule ambao fans wake walikuwa wakiumis. Katika tuzo za Grammy juzi kati Cool J alifanya bonge la show na kuweza ku perfom live ngoma hii. Kama wapenda real hip hop, then hii ndo albam yako.

Friday, February 1, 2013

Hali ya afya ya Msanii wa Vichekesho 'Matumaini' ni mbaya

Hali ya afya ya Msanii wa maigizo na vichekesho nchini Tumaini Martin 'Matumaini' inasemekana kuwa ni mbaya. Kwasasa Inasemekana Matumaini yupo nchini Msumbiji ambako alienda kwaajili ya kujitafutia maisha. Na inadaiwa kuwa Msanii huyo anatafuta msaada wa kurudi nchini Tanzania, hana nauli wala msaada wowote. Hadi sasa haijajulikana ugonjwa unaomsumbua msanii huyo. Maelezo zaidi ingia hapa

Q Chillah- Butterfly mp3.

G Nako ft. Ben Pol-Mama Yeyo mp3.

Ben Pol ft. Linnah-Yatakwisha mp3.

Baada ya ngoma ya Samboira, chukua zouk jingine hili hapa kutoka kwa mkali Ben Pol akiwa amemshirikisha mdada Linah. 'Yatakwisha' ndo jina la wimbo.

Wednesday, January 30, 2013

Rihanna afunguka rasmi kuwa wamerudiana na Chris Brown

Mwanadada Rihanna ameweka wazi kuwa yeye na Chris Brown kwasasa wameamua kurudisha mapenzi yao kama zamani. Akiongea na Rolling stone Riri amesema kuwa anaamini Brown hawezi kumfanyia tena kama yale aliyomtendea mwaka 2009 yaliyopelekea kuvurugana. Amesema kuwa kwasasa wamebadilika sana sio kama zamani. "You see us walking somewhere, driving somewhere, in the studio, in the club, and you think you know. But it's different now. We don't have those types of arguments anymore. We talk about sh--. We value each other. We know exactly what we have now, and we don't want to lose that."
Bac sawa!!!

Fabulous arudi upya,aahidi makubwa kwenye album ijayo ya 'Loso's way2'

Mkali wa Rap, Fabulous ameibuka na kusema kuwa kwasasa yupo kwenye hatua za mwisho katika kukamilisha albamu yake yenye muendelezo wa albamu yake namba moja ya 'Loso's way' ya 2009.Albamu hii anaiita 'Loso's way2'. Amefunguka hayo kupitia Billboard na amesema albam hiyo amewashirikisha wakali kibao kama vile Rick Ross, Chris Brown, John Legend, Neyo, Trey songz na wengine wengi.

RICK ROSS SASA KULINDWA NA WALINZI 24

Mkali na kiongozi wa MMG Rick Ross, hivi sasa inasemekana ameamua kuajiri walinzi 24 kufuatia kukoswakoswa na risasi juzi kati. Lakini wadadisi wa mambo wanadai kuwa Rossay alishakuwaga na walinzi idadi hiyo tangu kitambo, ila kikubwa kinachoonekana sasa ni kuwa hawa walinzi wake wasasa inasemekana ni majamaa ambao ni ma professional katika kutupa michomo ya bunduki na pia inawezekana wakawa ni wanajeshi wastaafu. Duuuu!! Bongo baadae sana.

Tuesday, January 29, 2013

Fid Q aweka hewani Beats alizowahi tumia, asema ruksa kuzitumia kama unauwezo

Mkali Fareed Kubanda, Fid Q ameweka wazi kuwa kama kuna Mc yeyote anayehitaji kutumia beats ambazo yeye alishazitumia ni ruksa. Ameyasema hayo leo kupitia akaunti yake ya facebook. Anahitaji ma MC wenye uwezo wa kuzitendea haki beats zake. Unaweza kuzipata hizo beats kwa kubonyeza HAPA
Kazi ni kwenu watuwangu ambao huwa mnalalamika hamna hela ya kugonga beat. Ni muda wenu wa kuonesha uwezo.

Sunday, January 27, 2013

Nikki Mbishi asema wimbo wake utaitwa 'NEY WA MITEGO' atoa mistari kadhaa Facebook.

Kupitia page yake ya facebook Nikki Mbishi 'Baba Malcolm' leo kaibuka na Post hii hapa chini. Hebu isome mwenyewe pamoja na comment za wadau then tafakari. Ukipata jibu niambie itamuweka katika mazingira gani na msanii mwenye jina linalo fanana na jina la wimbo wake. Siongei saaana.




    • Fredy Rafael Nikki Mbish ney asije akaanzisha bifu la mwaka
    • Amina Hassan Kijana mbn kam unaanza chokochoka mtaonana wabaya muda c mrefu
    • Paul Francis Ha ha ha ha ha ha haaa hii ni hatariiiiiiiiiii.........
    • Scrank Dapa Slopadanga Ney hawez vumilia, nazan unatafuta bifu maana cjui ka ataelewa kama 2lvoelewa sis
    • Sebastian James Jr. mmmhhhhhh we subir vumbi la hyooo muhun mwehu maaana dah
    • Joel Ndanzi Mmmmmmmh! Mvua ya ugomv hiyoooooo!
    • Sindato Conscious oiii!!! xaxa unataka kubakwa nick mbxh
      Hope Lee Duh... Meipenda iyo!
    • Dallarz Ukuni Duuh!ushauri wa bure achana na bifu za namna hiyo cz inaweza ikafanya watu wakuarafat bure mji uuone mchungu
    • Issa Mwalimu Aisee idea ni nzuri ila nahis bifu nzito inakuja
    • Saleh Kawambwa Ucpende cfa za kijinga!
    • Tamka Samweli idea nzuri lakini jina la wimbo sio kaka,achana nalo coz utakumbana na beef zsizo na maana

    • Aloyce Këšşý wamekuchokoza midomo imeponza vichwa its over niko soba nasiko chicha
    • Shomary Omary Babuu Kip it rily... f**k dem wack mc'z til dem drop. Fear none RESPECT few BROZA.