Saturday, December 3, 2011

Mr. Ebo, hautasahaulika kame

Ni habari ya kusikitisha ya kumpoteza msanii pekee ambaye alikuwa wa kwanza kudumisha utamaduni wa kabila lake kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya. Kikubwa ni kwa wasanii mliobaki kuiga mfano wa Mr. Ebbo. Mkataa kwao ni mtumwa. Achaneni na umagharibi.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Saturday, November 12, 2011

MITUTU NDIO SULUHISHO?????

Sometime unapofikiria unaweza kukosa jibu kwamba ni jitihada za kuwakomboa wananchi au kuwakandamiza, hususan pale kwenye masuala ambayo viongozi wanadai ni ya maendeleo. Angalia chanzo cha haya matatizo then pima na njia zinazo tumika kuyatatua. Hili lililotokea mbeya linafanana na lile lililotokea Mwanza hivi karibuni. Na matukio yote mawili yamesababishwa na mtu mmoja "MR. Kandoro " na sera zake za safisha jiji. Kafanya mwanza yametokea maafa, sasa kayaleta mbeya maafa mengine. Ni sera nzuri lakini mheshimiwa anakosa approach zenye ushirikiano na wananchi wake. Maoni tu.

Sunday, October 16, 2011

HILI NDO JEMBE, BELIEVE ME

UNAWAKUMBUKA DPT?

Bongo hiphop icon that will never be forgotten. Do u know where are they and what they do? Stay tuned

 

BELLA KOMBO: CHAGUO LA WENGI BSS 2ND CHANCE ALIYESTAHILI TUZO NA AKANYIMWA

Shindano la BSS Second chance limeisha kwa kuwashangaza wengi kwa kutupwa nafasi ya mwisho mwanadada pekee ambaye alionesha kipaji kikubwa Bella kombo.

Maoni ya wengi yanaonesha mashaka ya maamuzi ya mwisho. Anyway, hao ndo majaji ambao wanasema wao ndo wenye asilimia 60 za maamuzi na 40 za watazamaji, sasa kama ndo hivyo si wangemaliza zote tu.

Hata hivyo experience inaonesha kuwa wanaopewaga tuzo BSS huwa hawadumu hewani. Mtu kama Kala Jeremiah bado ana shine kwenye game,yuko wapi J4 na waliofuata?

Sunday, October 9, 2011

Professor Jay 2002 VS Ace Hood 2011


Profesa Jay alitoa album ya machozi jasho na damu miaka mingi iliyopita, cha ajabu mwaka huu 2011 Mkali Ace hood katoa album iitwayo Blood, Sweat and Tears ambayo inatafsiri kile alichokisema prof miaka kibao iliyopita.sasa je, ingekuwa vp kama angeanza Ace hood then afuatie Prof? Najua mngesema mengi. By the way Title sio ishu,angalia kazi.