Sunday, August 26, 2012

50 Cent - Be My Bitch feat Brevi (Official Music Video)

Friday, August 24, 2012

B.O.B NA NICKI MINAJ WAMETISHA KWENYE VIDEO YA 'OUT OF MIND'

Wakali B.O.B na Nicki Minaj wametisha ilembaya katika video ya 'Out Of Mind'ambapo inaanza kwa kumuonesha Bobby ray akiwa amefungwa na amevishwa mavazi ya wagonjwa wa akili,na kupitia kamera za usalama za hospitali anaonekana bob akipiga ukuta huku
akijitahidi kuyatoa mavazi meupe aliyovalishwa, katika kipande kingine mchizi anasikika aki rap maneno haya "Don't look at me wrong, I'm out of my mind, Nostradamus and da Vinci combined/ So paranoid of espionage, I'm watchin' my doors and checkin' my blinds," kisha kama bahati hivi B.O.B anapata rafiki ambaye ni Dokta Minaj Nicki, na wakati wa mahojiano ya mgonjwa na dokta, minaj analitoa koti lake jeupe na kuanza ku rap maneno akimwambia Bob "You gonna really need a wish right now when my goons start shootin' stars." Ni bonge ya video ambayo hupaswi kuikosa kuiona na ndio maana nimekutupia hapa chini uichukue. Enjoy.

CATRINA - KARIBU YANGU (OFFICIAL VIDEO)

MICHAEL Feat. AMINI & AT -TUNAFANYA MAMBO (OFFICIAL VIDEO HD)

Thursday, August 23, 2012

'FREELANCERS' MOVIE MPYA YA 50CENT

Hii ni Bonge ya movie kutoka kwa mkali 50Cent akiwa na mkali Forest Whitaker aliyewahi kucheza filamu ya Idd Amin ijulikanayo kama 'Last king of scotland'. Tayari ipo sokoni waweza jipatia kopi yako.

Friday, August 17, 2012

DULLY SYKES - MTOTO WA KARIAKOO (OFFICIAL VIDEO)

RICK ROSS AACHIA 'AMSTERDAM' VIDEO

Rapa  Rick Ross ameachia video mpya kutoka katika albam yake mpya iitwayo 'God forgives,I dont'.
Wimbo unaitwa 'Amsterdam' na video imeongozwa na Dre films. Humo ndani wamo wakali kadhaa kama vile Tyga na Omarion. Alipokuwa akiongelea video hiyo Rossy ambaye pia ni Boss wa MMG amefunguka kuwa video ime base katika 'red light district', na alipoulizwa ni kwanini ime base huko alifunguka kama ifuatavyo: ‘I kinda flipped it where being a boss you gotta get approval for a greenlight’.
‘I’m one of those people you can’t green light. As long I’ve been in this game, there’s been a lot of talk, but ain’t nobody stepped on these 11 and a half’s. The reason being: This is the red light district, you can’t move on this side.’ Ni bonge moja la video. Itupie jicho hapa chini.






HATIMAYE ROBIN VAN PERSIE KUTUA OLD TRAFORD

Inaonesha Babu Ferguson ameshinda mbio za kumchukua RVP, na kwa mantiki hiyo mchezaji huyo anatarajiwa kukipiga na mashetani wekundu na kuachana na Arsenal.Kweli chema chajiuza. All the best RVP.

Thursday, August 16, 2012

NICKI MINAJ AMFAGILIA FOXY BROWN,ASEMA NDIYE PEKEE ALIYEMVUTIA KUINGIA KWENYE GAME

Mwanadada Nicki minaj kutoka YMCMB ameweka wazi kuwa msanii pekee aliyemfanya avutike kwenye game la muziki ni mwanadashosti Foxy Brown.
Ameyasema hayo alipokuwa kwenye steji na kumpandisha stejini Foxy kisha kufunguka live kuwa Foxy ndiye msanii pekee aliye mu-influence kwenye game hii ya hip-hop. Wakiwa stejini Minaj alisikika akimpa asante Foxy kwani ndiye aliyemfanya awepo hapo alipo "I really wanna thank you for being one of my biggest influences in the game,""For her to be on my stage, it was emotional, and she was emotional,"  "This is what this is really about. When you get where you have arrived to, you give thanks to people who opened those doors and triggered something in your mind. When I found out Foxy Brown was from Trinidad, that did something to me. In my mind, I felt like I could be proud of where I'm from." Alisema Nicki.

DRAKE NA CHRIS BROWN WAPIGWA FAINI YA DOLA MILIONI 16

Wakali Drake na Chris Brown wamepigwa faini ya dola za kimarekani milioni 16 Kutokana na ugomvi kati yao uliotokea Juni 14 mwaka huu na kusababisha takribani watu 7 kuumizwa.
Washikaji wamekumbwa na faini hii jumatano jana baada ya mahakama kuona kuwa wanastahili kulipa kutokana na hasara iliyotokea usiku wa tukio katika klabu ya W.I.P.

The Expendables 2, KUZINDULIWA RASMI KESHO

Ni bonge la movie ambalo kwa mpenda action huwezi kuthubutu kuikosa. Inajumuisha wababe kibao akiwemo Sylvester Stallone 'Rambo', Jean Claude Van Damme, Jason Stathan, Chuck Norris na wakali wengine kibao.
Mpango mzima unazinduliwa kesho na baada ya hapo ni sokoni kama kawa tujibebee kopi.

Professor Jay ft Dully Sykes - Hellow.mp3



Sunday, August 12, 2012

NEY WAMITEGO NA SINTA NDANI YA BIFU

Juzi kati kupitia kipindi cha runinga cha Clouds tv kiitwacho Take One ambacho kime base zaidi katika kufanya mahojiano na masupastaa wa bongo movie, kilikuwa meza moja na mkali wa bongo flavour Nay wamitego, ambaye katika single yake iitwayo 'Nasema nao'amewachana mademu wa bongo movie kavukavu kuwa wengi wao ni malaya. Nay ameenda mbali zaidi baada ya kumtaja live mwanadada Christina a.k.a Sinta kuwa ni mmojawapo ya wasanii ambao wako tayari kufanya kitu chochote ilimradi aweze kung'ara tena katika gemu. Baada ya kutajwa na Nay, Mdada Sinta naye kupitia mtandao wake ameamua kujibu kwa kumchana kavukavu mchizi Nay.Swali langu ni kwamba, hivi ni sawa kwa wasanii kupakana live kihivi? KAAAAAAZI KWELI KWELI. Hii stori ni kwa msaada wa DJ Fetty

RIHANNA AFUNGUKA KWA OPRAH WINFREY JUU YA CHRIS BROWN, ASEMA AMEPOTEZA 'BEST FRIEND'

Mwana da-shosti Rihanna amefunguka kupitia kipindi cha mwanamama Oprah Winfrey kuwa kutokana na kutengana kwake na mkali Chris Brown anahisi kama amempoteza rafiki wake kipenzi 'best friend'. Rihanna kwenye mahojiano hayo anaonekana kutosita kuonesha hisia zake juu ya Chris Brown. Kutokana na hayo watabiri wa mambo wanahisi wapenzi hawa wa zamani Chris na Rihanna kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kurudiana.
 Hii ni Teaser kutoka kwa Mwanamama Oprah juu ya Next Chapter ambayo itaenda hewani kuanzia August 19.

TAKE OFF - GNAKO ft AY & The Artist

LEFT & RIGHT - MAWAZO

AMIRADO - BAHARI

DAN ROCK feat. MAUNDA ZORRO - MUDA UMEWADIA (OFFICIAL VIDEO HD)

AT-BI. HARUSI

Tuesday, August 7, 2012

MWANDISHI WA HABARI MOHAMED MASENGA, AINGIA KWENYE SIASA KISARAWE

Mwandishi wa habari, Mohamed Masenga, ameamua kubadili upepo na kuanza kujishughulisha na mambo ya kisiasa. Mwandishi huyo ameonekana akichukua fomu ya kugombea nafasi ya ujumbe wa halmashauri kuu UVCCM Taifa ( NEC ) pande za kisarawe. Kama inalipa all the best kaka. Siasa njema.

MUWEZESHE 'CATRINA' FIESTA SUPA NYOTA 2012

Tuma neno FIESTA 14 kwenda namba 15678 kumpigia kura Catrina ashinde katika fiesta supa nyota 2012.Ni mdada mkali wa sauti kutoka A-town. Anaweza.

Nuh - Bwege Mtozeni ( DarStamina International )

Dogo Janja ft. PNC - Ya Moyoni (Official Video)